<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<feed xmlns="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/">
<title>Department of Kiswahili &amp; Other African Languages</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/105" rel="alternate"/>
<subtitle/>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/105</id>
<updated>2026-05-15T12:09:21Z</updated>
<dc:date>2026-05-15T12:09:21Z</dc:date>
<entry>
<title>Kuchunguza Sababu Zinazowalazimu Wahusika Kufanya Ukahaba katika Riwaya ya Nyota ya Rehema Na Ndoto ya Almasi</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/6136" rel="alternate"/>
<author>
<name>Deusdedit, Karuhanga</name>
</author>
<author>
<name>Indede, Florence Ngesa</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/6136</id>
<updated>2024-08-05T13:17:25Z</updated>
<published>2023-05-01T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Kuchunguza Sababu Zinazowalazimu Wahusika Kufanya Ukahaba katika Riwaya ya Nyota ya Rehema Na Ndoto ya Almasi
Deusdedit, Karuhanga; Indede, Florence Ngesa
Utafiti huu ulichunguza suala la ukahaba katika riwaya ya Nyota ya Rehema (Mohamed S.Mohamed) na Ndoto ya Almasi (Ken Walibora). Kitendo cha ukahaba kimesababisha mashaka mengi sana katika maisha ya mwanadamu kama vile kupoteza ujira, uharibikaji wa ndoa, maradhi ya zinaa, vifo, kukata tamaa na utengano miongoni mwa wanajamii. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa ni: kubainisha usawiri wa ukahaba na wahusika makahaba katika riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi; kuchunguza sababu zinazowalazimu wahusika kufanya ukahaba katika riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi; na kudhihirisha athari za ukahaba kwa wahusika waliomo katika riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi.  Mtafiti alitumia nadharia ya utekelezi ambayo ni miongoni mwa nadharia nyingi zenye mtazamo wa kisosholojia. Nadharia ya utekelezi imeendelezwa na wanasosholojia kama vile Talcort Parsons na Emile Durkheim kama wanavyonukuliwa na Worsely Introducing Sociology (1970), huku akisema kwamba ukahaba husababishwa na mambo mawili yaani haja ya kutekeleza mahitaji ya kiuchumi na kwa kukidhi matashi ya nafsi zao kiashki.  Mtafiti pia alitumia nadharia ya umaksi iliyoanzishwa na Karl Marx (1818-1863) na Fredrich Engles(1820-1895).  Nadharia hii hufaa utafiti huu kwa kudhihirisha wahusika wanaoshiriki katika vitendo vya ukahaba kwa ajili ya kupata fedha au zawadi. Mabepari au walionacho huwa na lengo la kuridhisha miili yao tu na wanyonge huwa na lengo la kupata pesa ili kutimiza mahitaji yao, pengine, mnyonge hutolea mwili wake kwa ajili ya kupewa kazi au kupandishwa cheo kazini au kama njia ya kuilinda kazi yake ili asipigwe kalamu. Utafiti huu ni wa maktabani kwa hivyo, maktaba yaliyotumika ni yale ya Chuo Kikuu cha uislamu kilichopo nchini Uganda, Chuo kikuu cha Bishop Stuart Mbarara, na maktabani ya shule ya upili Heritage. Data za utafiti huu zilikusanywa kutoka maktabani kwa kutumia mbinu ya usomaji makini na uchunguzaji wa riwaya teule yaani: ile ya Nyota ya Rehema na ya Ndoto ya Almasi kwa kuzisoma na kuzichambua kwa kina na kuiwasilishwa data kwa mbinu ya kiuthamano. Utafiti huu umebainisha kuwa wahusika hufanya ukahaba ili kupata pesa au kuridhisha matashi ya nafsi zao kiashiki. Utafiti huu utakuwa wa muhimu sana kwa kufunza jamii kwamba kahaba si mwanamke peke yake kama inavyochukuliwa katika baadhi ya jamii bali kahaba ni mtu yeyote awe mwanamume au mwanamke anayeshiririki vitendo vya uzinzi.
DOI: https://doi.org/10.37284/jammk.6.1.1194
</summary>
<dc:date>2023-05-01T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>The Application of Mathematical Formulas in Teaching Linguistics Among STEM Learners in Higher Learning Institutions</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/6127" rel="alternate"/>
<author>
<name>Okal, Benard Odoyo</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/6127</id>
<updated>2024-07-31T13:55:55Z</updated>
<published>2024-01-01T00:00:00Z</published>
<summary type="text">The Application of Mathematical Formulas in Teaching Linguistics Among STEM Learners in Higher Learning Institutions
Okal, Benard Odoyo
The chapter focuses on mathematical formulas used to teach linguistics aspects amongst STEM learners. Though mathematics is used in teaching sciences and technology-related disciplines, its formulas are also applicable in teaching arts and social sciences such as linguistics, geography, history, economics, fine arts, commerce, psychology, physical education, sociology, political science, anthropology, public policy, and communication studies among others. Mathematical formulas applicable in teaching selected aspects of linguistics to STEM-inclined learners include sonority scale index and XY axis (for phonetics and phonology); tree diagrams and basic square roots (for morphology and syntax); mnemonics and word root schemata (for vocabulary learning); equal sign (a = b) (for synonymy analysis); pictograms (for polysemy); exponential formula (xn) (for the presentation of homonyms); number lines (for gradable antonyms); and set theory formula, arithmetic addition (X+Y), and X is greater than Y (for meronymy and hyponymy presentation).
The article is found in the book titled: Addressing Issues of Learner Diversity in English Language Education&#13;
&#13;
DOI: 10.4018/979-8-3693-2623-7.ch011.
</summary>
<dc:date>2024-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Uhakiki linganishi wa taarifa muhimu kuhusu vidahizo katika kamusi ya karne ya 21 na kamusi ya Kiswahili sanifu</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/6126" rel="alternate"/>
<author>
<name>Okal, Benard Odoyo</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/6126</id>
<updated>2024-07-31T13:47:14Z</updated>
<published>2024-04-11T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Uhakiki linganishi wa taarifa muhimu kuhusu vidahizo katika kamusi ya karne ya 21 na kamusi ya Kiswahili sanifu
Okal, Benard Odoyo
Kamusi kadhaa wahidiya (za lugha moja) za Kiswahili kama vile Kamusi ya Kiswahili Sanifu toleo la kwanza, pili na tatu, zimewahi kutungwa kutokana na juhudi za Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) inayojulikana sasa kama Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) ili kusaidia mafunzo ya Kiswahili na taaluma ya leksikografia katika taasisi kadhaa za elimu. Kamusi nyingi wahidiya za Kiswahili zimetungwa kwa kutumia mitindo anuwai ya utoaji maelezo ya taarifa muhimu za vidahizo husika licha ya kwamba kuna lugha kienzo maalum ya kuzingatiwa katika kuwasilisha taarifa hizo za vidahizo. Hivyo basi, makala haya yanahakiki kiulinganifu wa taarifa muhimu kuhusu vidahizo katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu toleo la tatu (TUKI, 2013) na Kamusi ya Karne ya 21 (Mdee, Njogu na Shafi, 2011). Uhakikiki linganishi katika makala haya umehusisha masuala anuwai hasa maelezo ya idadi ya vidahizo, mpangilio wa vidahizo, taarifa za kisarufi (tahajia na matamshi, kategoria ya kidahizo, ngeli, uelekezi wa vitenzi, mofolojia hasa minyambuliko ya vidahizo, maana na matumizi ya vidahizo katika miktadha anuwai) pamoja na vipengee vingine vya lugha kienzo ya msimbo kwa mujibu wa taaluma ya leksikografia.
</summary>
<dc:date>2024-04-11T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Mitindo ya Lugha Inayowabainisha Wahusika Wazimu katika Riwaya za Habwe</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5841" rel="alternate"/>
<author>
<name>Odhong’, Joseph Ondiek</name>
</author>
<author>
<name>Amukowa, Debora Nanyama</name>
</author>
<author>
<name>Asiko, Beverlyne  Ambuyo</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5841</id>
<updated>2023-11-08T17:01:55Z</updated>
<published>2023-07-31T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Mitindo ya Lugha Inayowabainisha Wahusika Wazimu katika Riwaya za Habwe
Odhong’, Joseph Ondiek; Amukowa, Debora Nanyama; Asiko, Beverlyne  Ambuyo
Takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni zinaonyesha ongezeko la idadi ya wazimu katika jamii duniani kote (Kovacevic, 2021). Waandishi wa fasihi wamewaumba wahusika wazimu wakiakisi mazingira wanamoishi. Tangu jadi wahakiki wamejitahidi kueleza vipi wahusika wazimu wametumika katika fasihi. Tahakiki za tamthilia za Shakespeare na za Kiingereza za karne ya ishirini zimeeleza namna na sababu za uumbaji wao. Katika riwaya za Kiswahili hakuna tahakiki zinazoshughulikia wahusika wazimu wala mitindo ya lugha inayowabainisha. Makala hii ilidhamiria kuchanganua mitindo ya lugha inayowabainisha wahusika wazimu katika kazi teule za Habwe. Uteuzi huu ulitokana na Habwe kusifiwa kuwa mwandishi wa fasihi ya kiongofu aliyetumia motifu ya wazimu katika riwaya zake (Gromov, 2018). Riwaya tano za Habwe:  Paradiso (2005), Cheche za Moto (2008), Fumbo La Maisha (2009), Safari ya Lamu (2011) na Kovu Moyoni (2014) ziliteuliwa kupitia usampulishaji dhamirifu kwa kuwa zilikuwa na wahusika wazimu. Nadharia ya umitindo iliyoasisiwa na Bally (1909) ) na kuendelezwa na Thornborrow na Wareing (1998) iliteuliwa kwa ajili ya kazi hii. Muundo wa kiuchanganuzi umetumiwa. Data zilikusanywa kutumia kifaa cha kudondoa data kilichokuwa na vidokezo vya mitindo ya lugha inayotambulisha wahusika wazimu. Matini ya riwaya teule imesomwa kwa makini na vipengele mbalimbali, kurekodiwa. Kisha data imechanganuliwa, kufasiriwa na kuratibiwa kulingana na madhumuni ya utafiti. Matokeo yamewasillishwa kwa njia ya maelezo. Makala hii imedhihirisha jinsi mitindo ya lugha ilivyotumiwa kuwatambulisha wahusika wazimu.
https://doi.org/10.37284/jammk.6.1.1345
</summary>
<dc:date>2023-07-31T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5673" rel="alternate"/>
<author>
<name>Barasa Martin Mulwale, Ngesa Florence Indede, Asiko Beverlyne Ambuyo</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5673</id>
<updated>2023-04-24T17:12:45Z</updated>
<published>2023-03-27T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Barasa Martin Mulwale, Ngesa Florence Indede, Asiko Beverlyne Ambuyo
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufahamu na kutagusana na ulimwengu huhitaji matumizi ya kiisimu ya kipekee. Katika muktadha wa kidini kuna changamoto ya asili ya maneno, mamlaka, utambulisho na ushirikiano wa wahusika. Aidha, miktadha mbalimbali ya kidini hutumia lugha kutimiza mahitaji yake maalum. Lugha hutenda matendo, huomba maombi ya kukemea, husimulia hali za kijamii na hata huonekana kudhibiti matendo ya Maulana. Ni kwa misingi hii ndipo kazi hii inajukumika kutalii jinsi lugha ya Kiswahili na Kibukusu zinavyotagusana katika mawanda haya ya dini, hasa Dini ya Musambwa (DYM) ambayo inaaminika kuwa ya kiasili katika jamii hii ya Wabukusu katika Kaunti ya Bungoma. Kazi hii inazingatia misingi ya Spolsky (2004, 2006, 2009) ambaye anajadili kuwa sera ya lugha halisi ya jamii hupatikana kwenye matumizi yake. Anazingatia Mwelekeo wa ikolojia ya lugha uliozinduliwa na Haugen (1972) unaochunguza mwingiliano baina ya lugha na mazingira. Muundo wa kiuchanganuzi ulitumiwa. Kupitia uchunzaji wa kutoshiriki moja kwa moja mtafiti alihudhuria ibada na kunasa mazungumzo yao kwenye kanda ya kunasia sauti. Mazungumzo hayo yalinakiliwa na orodha ya uchunzaji ilitumiwa kubainisha na kueleza namna lugha ya Kibukusu na Kiswahili zilivyotumiwa katika shughuli za kanisa hilo. Hali ya kuchanganya na kubadili msimbo, utohozi na hata matumizi ya Kiswahili kwa Kibukusu haikuweza kuepukika. Utafiti huu unadhihirisha kuwa raslimali za lugha zilizopo katika ikolojia fulani huchagizana katika kukamilisha majukumu ya mawasiliano katika muktadha husika.
DOI: https://doi.org/10.37284/jammk.6.1.1147
</summary>
<dc:date>2023-03-27T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Kubainisha Usawiri wa Ukahaba naWahusika Makahaba katika Riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5672" rel="alternate"/>
<author>
<name>Karuhanga Deusdedit, Indede Florence,  Nanyama Deborah Amukowa</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5672</id>
<updated>2023-04-24T17:01:29Z</updated>
<published>2022-12-28T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Kubainisha Usawiri wa Ukahaba naWahusika Makahaba katika Riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi
Karuhanga Deusdedit, Indede Florence,  Nanyama Deborah Amukowa
Utafiti huu ulichunguza ukahaba  katika riwaya ya Nyota ya Rehema (Mohamed S.Mohamed) na Ndoto ya Almasi (Ken Walibora). Kitendo cha ukahaba kimesababisha mashaka mengi sana katika maisha ya mwanadamu kama vile kupoteza ujira, uharibikaji wa ndoa maradhi ya zinaa, vifo, kukata tamaa na utengano miongoni mwa wanajamii. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa ni: kubainisha usawiri wa ukahaba na wahusika makahaba katika riwaya ya Nyota ya Rehema na Ndoto ya Almasi; Mtafiti alitumia nadharia ya utekelezi ambayo ni miongoni mwa nadharia nyingi zenye mtazamo wa kisosholojia. Nadharia ya utekelezi imeendelezwa na wanasosholojia kama vile TalcortParsons na EmileDurkheim kama wanavyonukuliwa na WorselyIntroductiontoSociology (1970), huku akisema kwamba ukahaba husababishwa na mambo mawili yaani haja ya kutekeleza mahitaji ya kiuchumi na kwa kukidhi matashi ya nafsi zao kiashki.  Mtafiti pia alitumia nadharia ya umaksi iliyoanzishwa na Karl Marx (1818-1863) na FredrichEngles(1820-1895).  Nadharia hii hufaa utafiti huu kwa kudhihirisha wahusika wanaoshiriki katika vitendo vya ukahaba kwa ajili ya kupata fedha au zawadi. Mabepari au walionacho huwa na lengo la kuridhisha miili yao tu na wanyonge huwa na lengo la kupata pesa ili kutimiza mahitaji yao, pengine, mnyonge hutolea mwili wake kwa ajili ya kupewa kazi au kupandishwa cheo kazini au kama njia ya kuilinda kazi yake ili asipigwe kalamu. Utafiti huu ni wa maktabani kwa hivyo, maktaba yaliyotumika ni yale ya Chuo Kikuu cha uislamu kilichopo nchini Uganda, Chuo kikuu cha Kimataifa Metropolitan, na maktabani ya shule ya upili Heritage. Data za utafiti huu zilikusanywa kutoka maktabani kwa kutumia mbinu ya usomaji makini na uchunguzaji wa riwaya teule yaani: ile ya Nyota ya Rehema na ya Ndoto ya Almasi kwa kuzisoma na kuzichambua kwa kina na kuiwasilishwa data kwa mbinu ya kiuthamano. Utafiti huu umebainisha kuwa wahusika hufanya ukahaba ili kupata pesa au kuridhisha matashi ya nafsi zao kiashiki. Utafiti huu utakuwa wa muhimu sana kwa kufunza jamii kwamba kahaba si mwanamke peke yake kama inavyochukuliwa katika baadhi ya jamii bali kahaba ni mtu yeyote awe mwanamume au mwanamke anayeshiririki vitendo vya uzinzi
DOI: https://doi.org/10.37284/jammk.5.2.1005
</summary>
<dc:date>2022-12-28T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Phonemic Representation and Transcription for Speech to Text  Applications for Under-resourced Indigenous African Languages:  The Case of Kiswahili</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5499" rel="alternate"/>
<author>
<name>Awino, Ebbie ; Wanzare, Lilian; Muchemi, Lawrence ; Wanjawa, Barack ; Ombui, Edward ; Indede,  Florence ; McOnyango, Owen ; Okal, Benard</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5499</id>
<updated>2022-11-16T18:43:03Z</updated>
<published>2022-01-01T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Phonemic Representation and Transcription for Speech to Text  Applications for Under-resourced Indigenous African Languages:  The Case of Kiswahili
Awino, Ebbie ; Wanzare, Lilian; Muchemi, Lawrence ; Wanjawa, Barack ; Ombui, Edward ; Indede,  Florence ; McOnyango, Owen ; Okal, Benard
Building automatic speech recognition (ASR) systems is a challenging task, especially for under resourced languages that need to construct corpora nearly from scratch and lack sufficient training &#13;
data. It has emerged that several African indigenous languages, including Kiswahili, are technologically &#13;
under-resourced. ASR systems are crucial, particularly for the hearing-impaired persons who can &#13;
benefit from having transcripts in their native languages. However, the absence of transcribed speech &#13;
datasets has complicated efforts to develop ASR models for these indigenous languages. This paper &#13;
explores the transcription process and the development of a Kiswahili speech corpus, which includes &#13;
both read-out texts and spontaneous speech data from native Kiswahili speakers. The study also &#13;
discusses the vowels and consonants in Kiswahili and provides an updated Kiswahili phoneme &#13;
dictionary for the ASR model that was created using the CMU Sphinx speech recognition toolbox, an &#13;
open-source speech recognition toolkit. The ASR model was trained using an extended phonetic set &#13;
that yielded a WER and SER of 18.87% and 49.5%, respectively, an improved performance than &#13;
previous similar research for under-resourced languages.
</summary>
<dc:date>2022-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Mitindo ya Lugha Inayomsawiri Mwanamke Kiongozi katika Tamthilia za Pango (2003) na Kigogo (2016)</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5416" rel="alternate"/>
<author>
<name>Ogonda S Sinzore, Deborah N Amukowa, Beverlyne A Ambuyo</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5416</id>
<updated>2022-10-16T13:27:19Z</updated>
<published>2021-01-01T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Mitindo ya Lugha Inayomsawiri Mwanamke Kiongozi katika Tamthilia za Pango (2003) na Kigogo (2016)
Ogonda S Sinzore, Deborah N Amukowa, Beverlyne A Ambuyo
Tafiti nyingi zilizofanywa kumhusu mhusika mwanamke katika tamthilia za Kiswahili zilimsawiri mwanamke kwa ujumla bila kuangazia uongozi wake. Chache zilizoshughulikia mwanamke kiongozi zimefanya hivi bila kuangazia mitindo ya lugha inayochangia kujenga taswira ya mwanamke kiongozi. Mitindo ya lugha ni muhimu katika kuibua maudhui ya kazi ya fasihi. Makala hii ililenga kuchanganua mitindo ya lugha inayomsawiri mwanamke kiongozi katika tamthilia za Pango (Wamitila, 2003) na Kigogo (Kea, 2016). Zimelengwa tamthilia hizi kwa kuwa zimeandikwa baada ya mwaka 2000 ambapo hadhi ya mwanamke kiongozi imeendelea kuimarika na jamii kuonekana kukubali uongozi wa mwanamke. Tamthilia za Pango na Kigogo ziliteuliwa kupitia mbinu ya usampulishaji dhamirifu kwa kuwa zina wahusika wanawake ambao ni viongozi. Nadharia ya Udenguzi iliyoasisiwa na Derrida (1966) na kuelezwa na Ntarangwi (2004) iliteuliwa kwa ajili ya utafiti huu. Mbinu ya uchanganuzi wa yaliyomo (maudhui) ilitumiwa kukusanya data. Tamthilia teule zilisomwa na data kunukuliwa. Data ilipangwa kisha ikachanganuliwa kwa njia ya uhakiki wa yaliyomo. Matokeo yamewasilishwa kwa njia ya maelezo. Imebainika kupitia makala hii kuwa mitindo mbalimbali ya lugha imechangia kujenga taswira ya mwanamke kiongozi katika tamthilia za Pango na Kigogo.
</summary>
<dc:date>2021-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Athari za Kimofosintaksia za Ngeli za Luganda katika Matumizi ya Kiswahili Sanifu Miongoni mwa Wanafunzi Shuleni, Uganda</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5415" rel="alternate"/>
<author>
<name>Mulei Martin, Debora Nanyama, Beverlyne Ambuyo</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5415</id>
<updated>2022-10-16T13:13:09Z</updated>
<published>2021-01-01T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Athari za Kimofosintaksia za Ngeli za Luganda katika Matumizi ya Kiswahili Sanifu Miongoni mwa Wanafunzi Shuleni, Uganda
Mulei Martin, Debora Nanyama, Beverlyne Ambuyo
Makala hii inaonesha athari za kimofosintaksia za ngeli za Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Makala hii inatokana na kuwa, Luganda na Kiswahili huainisha ngeli kutumia mfumo mmoja na matumizi yake kuzingatia sheria za kuonyesha upatanishi wa kisarufi wa nomino na maneno mengine katika tungo kimofosintaksia. Uwiano na tofauti za kanuni za matumizi ya vipashio vya kimofosintaksia baina ya lugha asili na Kiswahili sanifu umeripotiwa kuingiliana na kuathiri matumizi ya Kiswahili sanifu. Utafiti huu ulifanywa baada ya kubaini kuwa maandishi na mazungumzo ya wanafunzi ambao lugha yao ya kwanza ni Luganda na ambao wanajifunza Kiswahili kama lugha ya pili ulikiuka utaratibu wa kisarufi wa matumizi ya Kiswahili sanifu. Data ilitokana na uchanganuzi wa maandishi na mazungumzo ya wanafunzi 117, usaili na mijadala ya walimu 30 kutoka shule za upili 15 teule, wilayani Kampala, Uganda. Utafiti huu uliongozwa na mihimili ya sarufi bia na upatanifu wa nadharia ya Umilikifu na unganifu (Chomsky, 1981) ambayo huonesha ubia wa lugha na hali ya vipashio fulani vya kisarufi kutawala vipashio vingine katika tungo. Matokeo ya tathmini ya kanuni za matumizi ya kipashio cha kimofosintaksia cha ngeli za Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu yalidhihirisha athari za; uhamishaji wa maumbo, mofofonolojia, ubebaji wa viambishi vya ngeli tofauti, uchopekaji wa viambishi, ubadilishanaji wa viambishi ngeli, uchanganyaji wa maumbo na ujumlishaji wa viambishi vya msingi vya ngeli ya Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Makala hii inatarajiwa kuwasaidia walimu na wanafunzi kutambua athari za lugha ya kwanza katika matumizi ya Kiswahili sanifu, kuweka mikakati ya kuondokana na athari hizi kujenga matumizi bora ya Kiswahili sanifu.
https://doi.org/10.37284/eajss.3.1.331
</summary>
<dc:date>2021-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
<entry>
<title>Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma</title>
<link href="https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5414" rel="alternate"/>
<author>
<name>Mulwale, Barasa, Ngesa, Florence, Indede,  Asiko,Beverlyne Ambuyo</name>
</author>
<id>https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5414</id>
<updated>2022-10-16T13:05:19Z</updated>
<published>2022-01-01T00:00:00Z</published>
<summary type="text">Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Mulwale, Barasa, Ngesa, Florence, Indede,  Asiko,Beverlyne Ambuyo
Lugha ni chombo maalum katika ustawishaji na uimarishaji wa rasilimali za mwanadamu. Pia, ni wenzo unaohimili sera ambazo hulenga katika kutimiza matarajio ya kitaifa katika nchi yoyote ile. Nchini Kenya, vipengele katika katiba ya 2010, vinavyohusu lugha vilipandisha hadhi lugha ya Kiswahili ili iweze kutumika kama lugha ya taifa na rasmi sambamba na Kiingereza. Hata hivyo, katiba hii haijaweka kanuni zinazolenga kuimarisha na kudumisha uanuwai wa lugha za kiasili kote nchini Kenya. Machukulio ni kwamba, vipengele vya katiba vinasheheni sifa stahilifu kama vile, usawa wa kimatumizi, utekelezwaji, mikao ya kieneo, matakwa, pamoja na hiari za wananchi. Kwa kuangazia hali ya kiisimu-jamii katika Kaunti ya Bungoma, utata upo katika udumishaji wa mfumo ‘rasmi’ wa sera ya lugha Kitaifa, na utekelezwaji wa sera ya lugha kupitia asasi za serikali na zile za umma. Kazi hii inalenga kuchanganua uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu kupitia ruwaza zinazodhihirika katika mawanda mbalimbali ya lugha katika Kaunti ya Bungoma. Mihimili ya nadharia ya sera ya lugha iliyoendelezwa na Spolsky (2004, 2007) ambayo ni Usimamizi wa lugha na Ikolojia ya lugha pamoja na ruwaza za lugha ilivyoelezwa na Paltridge (2001) ndiyo nguzo ya kuchanganua utafiti huu.  Aidha, mtazamo wa Haugen (1972) unaohusu Ikolojia ya lugha umetumika katika kudhihirisha michakato baina ya lugha na mazingira inamotumika. Muundo mseto uliojumuisha, muundo wa kimaelezo, kiupelelezi na wa kiiktisadi ulitumiwa. Usampulishaji dhamirifu ulitumiwa kuteua matumizi ya lugha ya KS, KB na KS/KB katika ruwaza za lugha zilizodhihirika katika mawanda ya biashara, kanisani na utawala hasa kwenye mikutano ya umma au baraza za Chifu katika maeneo mbalimbali ya Kaunti ya Bungoma. Data ilikusanywa kwa kutumia mbinu ya uchunzaji usio-shirikishi na ya kiiktisadi ilikusanywa kwa kuhesabu hali ambazo lugha za KS, KB au KS/KB zilitumiwa. Ilibainika kuwa lugha ya KS na KB hukamilishana kiuamilifu katika mawanda mbalimbali ya kijamii katika Kaunti ya Bungoma.
DOI: https://doi.org/10.37284/jammk.5.1.665
</summary>
<dc:date>2022-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</entry>
</feed>
