• Login
    • Login
    Advanced Search
    View Item 
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Athari za Kimofosintaksia za Ngeli za Luganda katika Matumizi ya Kiswahili Sanifu Miongoni mwa Wanafunzi Shuleni, Uganda

    Thumbnail
    View/Open
    document (4).pdf (238.5Kb)
    Publication Date
    2021
    Author
    Mulei Martin, Debora Nanyama, Beverlyne Ambuyo
    Metadata
    Show full item record
    Abstract/Overview
    Makala hii inaonesha athari za kimofosintaksia za ngeli za Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Makala hii inatokana na kuwa, Luganda na Kiswahili huainisha ngeli kutumia mfumo mmoja na matumizi yake kuzingatia sheria za kuonyesha upatanishi wa kisarufi wa nomino na maneno mengine katika tungo kimofosintaksia. Uwiano na tofauti za kanuni za matumizi ya vipashio vya kimofosintaksia baina ya lugha asili na Kiswahili sanifu umeripotiwa kuingiliana na kuathiri matumizi ya Kiswahili sanifu. Utafiti huu ulifanywa baada ya kubaini kuwa maandishi na mazungumzo ya wanafunzi ambao lugha yao ya kwanza ni Luganda na ambao wanajifunza Kiswahili kama lugha ya pili ulikiuka utaratibu wa kisarufi wa matumizi ya Kiswahili sanifu. Data ilitokana na uchanganuzi wa maandishi na mazungumzo ya wanafunzi 117, usaili na mijadala ya walimu 30 kutoka shule za upili 15 teule, wilayani Kampala, Uganda. Utafiti huu uliongozwa na mihimili ya sarufi bia na upatanifu wa nadharia ya Umilikifu na unganifu (Chomsky, 1981) ambayo huonesha ubia wa lugha na hali ya vipashio fulani vya kisarufi kutawala vipashio vingine katika tungo. Matokeo ya tathmini ya kanuni za matumizi ya kipashio cha kimofosintaksia cha ngeli za Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu yalidhihirisha athari za; uhamishaji wa maumbo, mofofonolojia, ubebaji wa viambishi vya ngeli tofauti, uchopekaji wa viambishi, ubadilishanaji wa viambishi ngeli, uchanganyaji wa maumbo na ujumlishaji wa viambishi vya msingi vya ngeli ya Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Makala hii inatarajiwa kuwasaidia walimu na wanafunzi kutambua athari za lugha ya kwanza katika matumizi ya Kiswahili sanifu, kuweka mikakati ya kuondokana na athari hizi kujenga matumizi bora ya Kiswahili sanifu.
    Permalink
    https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5415
    Collections
    • Department of Kiswahili & Other African Languages [38]

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback

     

     

    Browse

    All of Maseno IRCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Statistics

    View Usage Statistics

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback