Show simple item record

dc.contributor.authorMULEI, MARTIN
dc.date.accessioned2023-08-04T07:34:13Z
dc.date.available2023-08-04T07:34:13Z
dc.date.issued2023
dc.identifier.urihttps://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5767
dc.description.abstractKiswahili ni lugha ya Kibantu yenye mifumo na miundo ya kiisimu ambayo ina upekee wake. Upekee huu husababisha tofauti za kiisimu na lugha nyinginezo za Kibantu kimuundo na kimfumo na kujenga athari za mwingiliano wa kimofosintaksia unaodhihirika katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Ingawa Kiswahili sanifu kinafundishwa shuleni nchini Uganda, matokeo ya matumizi yake yanadhihirisha athari za mwingiliano wa miundo na kanuni za vipashio vya kimofosintaksia vya Luganda katika maandishi na mazungumzo ya wanafunzi ambao L1 ni Luganda. Azma ya utafiti huu ilikuwa kuchanganua miundo na kanuni za mofosintaksia za Luganda na Kiswahili ili kubaini athari za mwingiliano wa utafiti huu ilikuwa: Kwanza, kufafanua jinsi vipashio vya kimofosintaksia vya Luganda sanifu hufanana na kutofautiana na vya Kiswahili sanifu. Pili, kuchanganua miundo na kanuni za mifanyiko ya kimofosintaksia ya Luganda na Kiswahili, tatu kutathimini athari za mwingiliano wa mofosintaksia ya Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Utafiti huu uliongozwa na mihimili miwili ya Ubia na Upatanifu ya nadharia ya Umilikifu na Unganifu ya Chomsky (1981). Mihimili ya sarufi bia na upatanifu ilizingatiwa katika kufafanua na kuchanganua kanuni za mofosintaksia ya Luganda katika Kiswahili sanifu. Muundo wa kimaelezo ulitumika katika utafiti huu. Utafiti huu ulifanyika katika kata tano za wilaya ya Kampala, Uganda. Ulijikita katika taaluma ya isimu linganishi na tumikizi. Ulichunguza jinsi isimu ya lugha za Kibantu huchangiana, kuingiliana na kuathiriana katika matumizi. Mbinu ya usampulishaji nasibu ilitumika kuteua shule 12 ambazo zinafundisha Kiswahili katika kidato cha sita. Mbinu ya kimaksudi na dhamirifu ilitumika kuwateuwa wanafunzi 54 wa kidato cha sita ambao L1 ni Luganda na watumiaji wa Kiswahili kama L2. Data ilikusanywa maktabani kwa kutumia mbinu ya uchanganuzi matini kutumia kifaa cha kudondoa data cha orodhahakiki chenye sifa za kimofosintaksia zinazotambulisha vipashio vya kimofosintaksia, miundo yake na kanuni za matumizi kudodoa data kulingana na malengo matatu ya utafiti. Nyanjani data ilikusanywa kutoka kwa wanafunzi kupitia kwa mijarabu na mijadala. Mijadala iliandaliwa kwa wanafunzi kujadili matokeo ya mijarabu ili kutathimini athari za mwingiliano wa kimofosintaksia wa Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu katika maandishi na mazungumzo shiriki. Data ilichanganuliwa na kuwasilishwa kutumia mbinu ya kimaelezo ikishirikisha majedwali na michoro kudhihirisha jinsi kanuni na miundo ya mofosintaksia ya Luganda inavyoingiliana na kuathiri matumizi ya Kiswahili sanifu miongoni mwa wanafunzi wa Kiswahili ambao L1 ni Luganda. Utafiti huu ulibaini kuwa licha ya Luganda na Kiswahili sanifu kuwa lugha za nasaba moja, ni lugha mbili tofauti za Kibantu zenye vipashio, miundo na kanuni za mifanyiko ya kimofosintaksia zinazofanana na kutofautiana. Uchanganuzi ulibaini athari za mwingiliano wa mofosintaksia ya Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Tathimini ya mwingiliano ulidhihirisha athari za uhamishaji, ujumlishaji, uchopekaji, udondoshaji, uchanganyaji, uongezaji wa fonimu na maumbo, miundo na kanuni za mifanyiko ya mofosintaksia ya Luganda katika matumizi ya Kiswahili sanifu. Athari hizi zilidhihirisha ukiukaji wa matumizi ya maumbo, miundo na kanuni za vipashio vya kimofosintaksia vya Kiswahili sanifu na kusababisha matumizi ya Kiswahili kisicho sahihi hasa katika mazungumzo na maandishi ya wanafunzi ambao L1 ni Luganda. Matokeo haya ni mchango mkubwa katika taaluma ya isimu linganishi ya lugha za Kibantu kwa kutambua athari za mwingiliano wa vipashio, miundo na kanuni za mifanyiko ya mofosintaksia ya Luganda kudhihirisha jinsi inavyoathiri matumizi ya Kiswahili sanifu, kukuza na kuendeleza umilisi na matumizi ya Kiswahili sanifu nchini Uganda. Utafiti huu ulipendekeza tafiti zaidi kufanywa kuhusiana na mwingiliano wa L1 katika matumizi ya L2 ili kuweka mikakati na misingi ya kukuza na kuendeleza umilisi na matumizi ya Kiswahili sanifu miongoni mwa wanafunzi unaotokana na mchango na athari za L1.en_US
dc.publisherMaseno Universityen_US
dc.titleUchanganuzi wa mofosintaksia ya Luganda katika matumizi ya kiswahili sanifu wilayani Kampala, Ugandaen_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record